CRISTIANO RONALDO NDANI KUPAMBANA NA MANCHESTER CITY



Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo yuko sawa kuchezea klabu yake dhidi ya Manchester City katika mechi ya nusufainali Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.


Mechi hiyo ya marudiano itachezewa Santiago Bernabéu kuanzia saa nne kasorobo usiku. Mechi ya kwanza ilimalizika 0-0.
Ronaldo, ambaye amefunga mabao 93 mechi za Ulaya, hakuweza kucheza mechi ya mkondo wa kwanza kutokana na jeraha misuli ya paja.
"Cristiano yuko sawa, 100%. Alishiriki mazoezi leo na atakuwepo kesho,” meneja wa Real Zinedine Zidane alisema Jumanne.

0 comments:

Post a Comment